Mechi za robo fainali kombe la CRDB zitaanza kutimua vumbi Jumamosi May 16 ambapo mechi mbili zitapigwa.
Coastal Union itaumana na Singida BS mchezo utakaopigwa saa 10 jioni kisha kufuatiwa na mchezo kati ya JKT Tanzania dhidi ya Yanga saa 12:30 jioni.
Jumapili Mashujaa Fc watacheza na Azam Fc saa 10 jioni na mechi ya mwisho kuzikutanisha Simba dhidi ya TRA United saa 12 jioni.




