Dube uso kwa uso na Fei Toto mbio za ufungaji bora

Joel JJ By Joel JJ • 4th May 2026


Dube uso kwa uso na Fei Toto mbio za ufungaji bora

Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube jana aliendeleza kasi yake ya kuzifumania nyavu akifunga bao la kwanza wakati timu yake ikitoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Simba katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo.

Bao hilo lilimfanya Dube afikishe mabao 9 sasa akilingana na kinara wa mabao Feisal Salum ambaye pia amefunga mabao 9.

Dube sasa amehusika katika mabao 13 ya Yanga akitoa pasi nne za mabao wakati Fei Toto akiongoza upande wa asisti pia akiwa nazo 8.

Dube amekuwa katika mwendelezo mzuri tangu alipopona majeruhi akiwa na wastani wa kufunga angalau bao moja katika kila mchezo.

 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.