Kikosi cha Singida BS kimeondoka visiwani Zanzibar kurejea Bara baada ya kutupwa nje ya michuano ya kombe la Muungano.
Jana Singida BS walikumbana na kipigo ambacho hawakukitarajia kutoka kwa Mlandege Fc wakichapwa mabao 2-1 katika mchezo wa robo fainali.
Singida BS ni timu pekee kutoka Bara ambayo haikufanikiwa kutinga nusu fainali baada ya Yanga, Azam Fc na Simba zote kutinga hatua hiyo.






