Kikosi cha Simba kimewasili visiwani Zanzibar tayari kwa michuano ya kombe la Muungano iliyoanza kutimua vumbi jana kwa mchezo wa kwanza wa robo fainali.
Wekundu wa Msimbazi watatupa karata yao siku ya kesho Alhamisi kwa mchezo dhidi ya Mafunzo utakaopigwa saa 2:15 usiku katika uwanja wa New Amaan Complex.
Endapo Simba itafuzu nusu fainali, itakutana na mshindi wa mchezo kati ya Singida BS dhidi ya Mlandege, mechi itakayopigwa mapema kesho.
Huu ni msimu wa tatu tangu michuano hiyo iliporejea ambapo Simba itakuwa ikisaka taji la pili baada ya kuibuka mabingwa katika msimu wa kwanza.







