Dirisha la usajili linazidi kunoga huku vilabu vikubwa Ulaya vikianza kuchukua hatua za mwisho kuelekea majira ya kiangazi. Hizi hapa ni tetesi kuu za leo kutoka vyanzo mbalimbali vya michezo:
Barcelona Wasita Kumchukua Rashford
Kwa mujibu wa Marca, FC Barcelona bado hawana uhakika kama watailipa Manchester United euro milioni 30 ili kumsajili Marcus Rashford kwa mkataba wa kudumu.
Anthony Gordon Aweza Kuondoka Newcastle
Ripoti kutoka The Telegraph zinaeleza kuwa Anthony Gordon yuko tayari kuondoka Newcastle United, huku Bayern Munich wakionyesha nia ya kumsajili.
Arsenal Wajiunga kwenye Mbio za Gordon
Kwa mujibu wa The Sun, Arsenal FC nao wameingia kwenye kinyang'anyiro cha Gordon, huku mchezaji huyo akipendelea kuhamia London.
Manchester City na Barcelona Wamnyatia Kinda wa Palmeiras
Ripoti za Daily Mail zinaonyesha kuwa Manchester City na FC Barcelona zinaongoza mbio za kumsajili Eduardo Conceicao wa Palmeiras.
Newcastle Yatarajia Mabadiliko Makubwa
Kwa mujibu wa The Sun, Newcastle United wanajiandaa kwa dirisha lenye shughuli nyingi, huku wachezaji kadhaa wa kikosi cha kwanza wakihusishwa na kuondoka.
Liverpool Inaweza Kuachana na Wachezaji Tisa
Ripoti kutoka The Telegraph zinaeleza kuwa Liverpool FC wanaweza kuwaacha wachezaji tisa, akiwemo Alexis Mac Allister na Joe Gomez.
Klopp na Pochettino Wawaniwa Real Madrid
Kwa mujibu wa Daily Mail, Jurgen Klopp na Mauricio Pochettino wanatajwa kuwa wagombea wa kuchukua nafasi ya kocha wa Real Madrid iwapo Alvaro Arbeloa ataondoka.
Matt Targett Afuatiliwa na Everton na Leeds
Teamtalk linaripoti kuwa Matt Targett, anayemilikiwa na Newcastle United lakini yupo kwa mkopo Middlesbrough FC, anafuatiliwa na Everton FC na Leeds United.
Tottenham Wapanga Kumuza Gallagher
Kwa mujibu wa Football Insider, Tottenham Hotspur wako tayari kumuuza Conor Gallagher licha ya kujiunga nao hivi karibuni.
Chelsea Kuwapa Mikataba Mipya Colwill na Caicedo
Ripoti kutoka The Times zinaeleza kuwa Chelsea FC wanapanga kuwapa mikataba mipya Levi Colwill na Moises Caicedo.
AC Milan Wamtaka Vlahovic
Kwa mujibu wa Gazzetta dello Sport, AC Milan wanamuwania Dusan Vlahovic kutoka Juventus FC.
Marseille Wamtaka Adam Aznou
Ripoti za Teamtalk zinaonyesha kuwa Olympique de Marseille wanavutiwa na Adam Aznou wa Everton FC.



