Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi, April 09 2026

Joel JJ By Joel JJ • 9th April 2026


Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi, April 09 2026

Dirisha la usajili majira ya kiangazi linakaribia huku vilabu vikubwa vikianza kuweka wazi malengo yao. Leo, taarifa zinaonyesha harakati kubwa za kuimarisha vikosi, hasa katika Premier League.


Arsenal Waimarisha Ulinzi

Arsenal wanatafuta kuongeza nguvu safu ya ulinzi kwa kulenga kumsajili Victor Valdepenas wa Real Madrid pamoja na Jacobo Ramon wa Como (CaughtOffside).


Martinelli Ang’ang’ania Kubaki Arsenal

Gabriel Martinelli ameweka wazi nia yake ya kuendelea kusalia Arsenal licha ya tetesi za kuuzwa (Football Insider).


Dortmund Wamtaka Tena Jadon Sancho

Borussia Dortmund wanapanga jaribio la tatu kumsajili Jadon Sancho, ambaye yuko kwa mkopo Aston Villa kutoka Manchester United (Telegraph).


Tottenham Wamnyatia Trafford

Tottenham Hotspur wanamtaka James Trafford wa Manchester City kama sehemu ya mipango yao ya usajili (TeamTalk).


Ada Kubwa kwa Elliot Anderson

Nottingham Forest wanataka kati ya pauni milioni 100 hadi 120 kwa Elliot Anderson, anayewindwa na Manchester United na Manchester City (Florian Plettenberg).


Everton Wajaribu Kumuweka Grealish

Everton hawako tayari kulipa pauni milioni 50 kwa Jack Grealish, lakini wanataka kubaki naye kutoka Manchester City (The Athletic).


City Wamfuatilia Kijana Eichhorn

Manchester City wamejiunga na mbio za kumsajili chipukizi Kennet Eichhorn wa Hertha Berlin (Fabrizio Romano).


Leeds Wamruhusu Mateo Joseph Kuondoka

Leeds United wako tayari kumuuza Mateo Joseph baada ya mkopo wake Mallorca (Football Insider).


Chelsea Wamkingia Kifua Acheampong

Chelsea hawana mpango wa kumuuza Josh Acheampong licha ya kucheza mara chache (Express).


Garnacho Aingia Kwenye Radar ya River Plate

Kocha Eduardo Coudet wa River Plate amewasiliana na Chelsea na Alejandro Garnacho kuhusu uwezekano wa mkopo wa mwaka mmoja (TyC / Football London).


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.