Slot aomba kuondoka Liverpool mwishoni mwa msimu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th April 2026


Slot aomba kuondoka Liverpool mwishoni mwa msimu

Kocha mkuu wa Liverpool, Arne Slot, ameanza safari ya kuhitimisha majukumu yake Anfield baada ya kusambaa ripoti kwamba ameutaarifu uongozi wa Liverpool atajiuzulu kama kocha wa klabu mwishoni mwa msimu huu.

Taarifa hizo zimeibuka kutoka kwa vyanzo vinavyohusiana moja kwa moja na mjadala ndani ya klabu na mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa leo, Slot amewasilisha rasmi wazo la kujiuzulu endapo masharti fulani ya makubaliano ya kifedha yatakubalika na uongozi wa Liverpool.

Pendekezo hili linaibuka huku msimamo wake ukipimwa upya kufuatia msimu mgumu wa 2025–26 ambao umejazwa na matokeo duni na msukosuko wa mafanikio ya klabu.

Liverpool walijikuta nje ya Kombe la FA Jumamosi iliyopita baada ya kupokwa 4–0 na Manchester City, tukio lililoipa timu wakati mgumu na kuongeza mashinikizo juu ya Slot kutokana na mfululizo wa matokeo yasiyo maridhawa.

Ripoti za vyombo vya habari zinaonyesha kuwa tayari mazungumzo juu ya hatima ya meneja huyo wa Uholanziyalishaanza huku mashabiki wengi wakionyesha kutoridhishwa na utendaji wa timu.

Licha ya kufanikiwa msimu uliopita kushinda ubingwa wa Ligi Kuu ya England, msimu huu umeonyesha kushuka kwa matokeo na ubora wa timu. Baadhi ya wanahabari na wachambuzi wa soka wanasema kazi ya Slot inaweza kufikia mwisho wake chini ya shinikizo kubwa la mafanikio kutokujidhihirisha kama ilivyotarajiwa.

Hata hivyo, uongozi wa klabu kwa sasa unaonekana kufanyia tathmini pendekezo lake kabla ya kuchukua uamuzi wa mwisho, huku baadhi ya ripoti zikieleza kwamba kocha huyo bado ana nafasi ya kufanikisha msimu huu katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.