Arsenal Waongoza Mbio za Kumsajili Tresoldi

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media β€’ 29th March 2026


Arsenal Waongoza Mbio za Kumsajili Tresoldi

Klabu ya Arsenal FC imepiga hatua kubwa katika mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji kijana wa Kijerumani mwenye umri wa miaka 21, Nicolò Tresoldi, kutoka Club Brugge./p>

Tresoldi alijiunga na Club Brugge majira ya kiangazi yaliyopita akitokea Hannover 96 kwa ada ya euro milioni 7.5, na tangu hapo ameonyesha kiwango bora katika msimu wake wa kwanza, akifunga mabao 17 katika mashindano yote.

Kwa sasa, Arsenal wanaonekana kuwa mbele ya klabu nyingine kutoka Hispania, Italia na Ujerumani katika mbio za kuwania saini yake, huku dili hilo likitarajiwa kugharimu kati ya euro milioni 25 hadi 30.

Uongozi wa Arsenal unaona usajili huo kuwa ni uwekezaji mzuri na wa gharama nafuu kwa ajili ya kuimarisha safu ya ushambuliaji ya kocha Mikel Arteta, akitarajiwa kuwa msaada kwa Gabriel Jesus na Kai Havertz ndani ya kikosi hicho.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.