Soko la usajili barani Ulaya linaendelea kupamba moto huku vilabu vikubwa vikisaka vipaji vipya au kuimarisha vikosi vyao kabla ya dirisha la majira ya joto. Hizi hapa ni tetesi kuu zinazotikisa vichwa vya habari leo:
Arsenal, City, United na Chelsea wamvizia Elliot Anderson
Kiungo wa Nottingham Forest, Elliot Anderson (23), ameibuka kuwa mmoja wa wachezaji wanaowindwa zaidi kwa sasa. Arsenal wanaongoza mbio za kumtaka, lakini wanakabiliwa na ushindani mkali kutoka Manchester City, Manchester United na Chelsea.
Chanzo: CaughtOffside
Manchester United wamfuatilia Adam Wharton
Manchester United wanaendelea kufuatilia kwa karibu kiungo wa England Adam Wharton (22), ambaye yuko tayari kuondoka Crystal Palace ili kujiunga na klabu inayoshiriki UEFA Champions League.
Chanzo: The Sun
Brighton wapunguza bei ya Carlos Baleba
Brighton & Hove Albion wameanza kulegeza msimamo wao kuhusu kiungo Carlos Baleba (22). Badala ya pauni milioni 100 walizokuwa wanadai, sasa wako tayari kusikiliza ofa ya chini zaidi.
Chanzo: The Sun
Mbio za Tchouameni zapamba moto
Kiungo wa Real Madrid, Aurélien Tchouaméni (26), anawindwa na Manchester United pamoja na Liverpool.
Chanzo: Fichajes
Arsenal na Liverpool wagonga mwamba kwa Kvaratskhelia
Arsenal na Liverpool wamepata pigo katika harakati zao za kumchukua winga wa Paris Saint-Germain, Khvicha Kvaratskhelia (25).
Chanzo: Teamtalk
Manchester United wapewa nafasi ya kumsajili Ferran Torres
Manchester United wamepewa nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa Hispania Ferran Torres (26) kutoka Barcelona msimu huu wa joto.
Chanzo: Teamtalk
Juventus wamuwania Lewandowski na Greenwood
Juventus wanataka kumsajili mshambuliaji mkongwe Robert Lewandowski (37) kwa uhamisho wa bure endapo ataondoka Barcelona.
Pia wanamfuatilia Mason Greenwood (24), lakini Atlético Madrid nao wanapambana kumsajili kutoka Olympique de Marseille.
Chanzo: La Gazzetta dello Sport
Luis Enrique aipa mgongo Manchester United
Kocha wa Paris Saint-Germain, Luis Enrique (55), anatarajiwa kukataa ofa ya Manchester United na badala yake kusaini mkataba mpya kuendelea PSG.
Chanzo: i Paper
Tottenham wafikiria Sean Dyche
Tottenham Hotspur wanaweza kumgeukia Sean Dyche (54) kusaidia timu kujinasua na hatari ya kushuka daraja, iwapo Roberto De Zerbi (46) ataendelea kushikilia msimamo wake wa kujiunga nao baadaye.
Chanzo: Telegraph
Everton wamtengea mkataba mpya Moyes
Kutokana na mafanikio ya kuibadilisha timu, Everton wanapanga kumpa kocha David Moyes (62) mkataba mpya baada ya kuibadilisha timu kutoka hatari ya kushuka daraja hadi ushindani wa nafasi za Ulaya.
Chanzo: Guardian



