Dirisha la usajili linazidi kupamba moto huku vilabu vikubwa Ulaya vikijipanga kwa ajili ya mabadiliko makubwa ya vikosi. Leo tunashuhudia majina mazito, dili kubwa zinazopikwa kimyakimya, na vita kali ya usajili kati ya miamba ya soka. Hizi hapa tetesi kuu za leo
Morgan Rogers awindwa na vigogo Ulaya
Kiungo mshambuliaji wa Aston Villa, Morgan Rogers (23), yuko tayari kujaribu maisha nje ya England.
Mabingwa wa Ulaya Paris Saint-Germain wameingia kwenye mbio hizo, wakishindana na:
- Arsenal
- Manchester United
- Chelsea
Chanzo: Talksport
Manuel Akanji kuelekea Inter Milan
Beki wa Manchester City, Manuel Akanji, anatarajiwa kujiunga na Inter Milan kwa ada ya euro milioni 15.
Chanzo: Fabrizio Romano
City bado wanamng’ang’ania Elliot Anderson
Manchester City wana imani kubwa ya kumsajili Elliot Anderson kutoka Nottingham Forest kwa dau linaloweza kufikia pauni milioni 100.
Chanzo: The Sun
Lorenzo Lucca kurejea Napoli
Mshambuliaji Lorenzo Lucca atarejea Napoli baada ya mkopo wake kumalizika, huku Nottingham Forest wakikataa kumnunua moja kwa moja.
Chanzo: Corriere dello Sport
Real Madrid yaonyeshwa Bernardo Silva
Wakala maarufu Jorge Mendes amemuweka sokoni Bernardo Silva wa Manchester City kwa Real Madrid.
Mkataba wake unamalizika Juni 30.
Chanzo: AS
Joao Gomes kwenye rada ya Atletico
Atletico Madrid wameanza mazungumzo na Wolverhampton Wanderers kuhusu Joao Gomes.
Ada yake inaweza kufikia pauni milioni 40.
Chanzo: Talksport
Marcos Senesi karibu na Tottenham
Beki wa Argentina Marcos Senesi amekubaliana kimsingi kujiunga na Tottenham Hotspur akitokea AFC Bournemouth kwa uhamisho wa bure.
Chanzo: Florian Plettenberg
Manchester United bado wanamtaka Rafael Leao
Manchester United ni miongoni mwa wanaomfuatilia Rafael Leao wa AC Milan.
Chanzo: Calciomercato
Manchester City wamuweka tayari mrithi wa Guardiola
Kocha wa zamani wa Chelsea, Enzo Maresca, anatajwa kuwa chaguo la Manchester City endapo Pep Guardiola ataondoka.
Chanzo: Fabrizio Romano
Kalulu aingia kwenye rada ya United
Juventus wanataka kuongeza mkataba wa Pierre Kalulu, lakini Manchester United wanamfuatilia kwa karibu.
Chanzo: Tuttomercatoweb
Van de Ven ataka kuondoka Spurs
Beki Micky van de Ven hataki kuongeza mkataba wake na Tottenham Hotspur na anatafuta changamoto mpya.
Chanzo: Teamtalk



