Baada ya Simba na Yanga kutoana jasho katika mchezo wa ligi kuu kukamilisha raundi ya 20 uliofanyika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo na kumalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 2-2 jana, ligi kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi za raundi ya 21 zitaanza.
Mapema saa 8 Mashujaa Fc watakuwa uwanja wa nyumbani Lake Tanganyika kuwakabili TRA United katika mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali.
Baadae mchezo huo utafuatiwa na Derby ya mkoani Mbeya, Tanzania Prisons wakiwakaribisha Mbeya City, mchezo utakaopigwa saa 10 jioni.




