Nyota wa soka wa Brazil, Neymar Jr., rasmi amerejea katika kikosi cha taifa cha Brazil kitakachoshiriki Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika Marekani, Canada na Mexico.
Kocha wa Brazil, Carlo Ancelotti, alitangaza kikosi hicho cha wachezaji 26 huku jina la Neymar likiwa gumzo kubwa kutokana na historia yake ya majeraha katika miaka ya karibuni.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Shirikisho la Soka Brazil (CBF), Neymar amerudi baada ya kukosa mechi nyingi za kimataifa tangu mwaka 2023 kutokana na majeraha ya goti.
Hata hivyo, Ancelotti amesema kuwa amemjumuisha kutokana na uzoefu wake mkubwa, uwezo wake wa kubadili mchezo, pamoja na maendeleo aliyoyaonyesha tangu kurejea kucheza akiwa na klabu ya Santos FC.
Mashabiki wengi wa Brazil wamepokea kwa furaha kurejea kwa Neymar, ambaye sasa atakuwa anacheza Kombe lake la Dunia la nne baada ya kushiriki michuano ya 2014, 2018 na 2022. Ancelotti anaonekana kuunda kikosi chenye mchanganyiko wa uzoefu na vipaji vipya ili kuisaka nyota ya sita ya dunia kwa Brazil. (reuters.com)
Kikosi cha Brazil cha Wachezaji 26 kwa Kombe la Dunia 2026
Makipa
- Alisson Becker
- Ederson
- Weverton
Mabeki
- Marquinhos
- Gabriel Magalhães
- Bremer
- Roger Ibañez
- Danilo
- Alex Sandro
- Wesley
- Douglas Santos
- Léo Pereira
Viungo
- Casemiro
- Bruno Guimarães
- Lucas Paquetá
- João Gomes
- Fabinho
- Andrey Santos
- Gabriel Sara
Washambuliaji
- Neymar Jr.
- Vinícius Júnior
- Raphinha
- Gabriel Martinelli
- Endrick
- Matheus Cunha
- Igor Thiago
Brazil ipo Kundi C pamoja na Morocco, Haiti na Scotland, na itaanza kampeni yake ya Kombe la Dunia tarehe 13 Juni 2026. Mashabiki wengi sasa wanaamini kuwa kurejea kwa Neymar kunaweza kuipa Brazil nguvu mpya katika harakati za kutwaa ubingwa wa sita wa dunia.



