Ligi Kuu ya NBC inazidi kuchanja mbuga ambapo leo mechi za raundi ya 19 zinatarajiwa kupigwa.
KMC wanaoburuza mkia kwenye msimamo wa ligi wanakutana na Tanzania Prisons ambao wanashikilia nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi.
Ni mechi ambayo kila timu inahitaji matokeo ili kujiimarisha katika vita ya mkiani wa msimamo.
Hata hivyo ni KMC wenye hali mbaya zaidi wakikusanya alama 8 tu kutoka mechi 18.




