England watangaza kikosi cha Kombe la Dunia 2026, Maguire aachwa nje

Joel JJ By Joel JJ • 22nd May 2026


England watangaza kikosi cha Kombe la Dunia 2026, Maguire aachwa nje

Kocha wa England, Thomas Tuchel, ametangaza rasmi kikosi cha wachezaji 26 kitakachoiwakilisha England kwenye Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika Marekani, Canada na Mexico.

Habari kubwa kwenye kikosi hicho ni kuachwa nje kwa beki Harry Maguire, ambaye alikuwa sehemu muhimu ya England katika mashindano makubwa ya nyuma. Maguire amesema amesikitishwa sana na uamuzi huo wa kuachwa nje ya kikosi.

Mbali na Maguire, nyota wengine walioachwa nje ni Phil Foden na Cole Palmer, huku mshambuliaji Ivan Toney akirejea kwenye kikosi baada ya kufanya vizuri katika ligi ya Saudi Arabia.

Kikosi kamili cha England – Kombe la Dunia 2026

Makipa

  • Jordan Pickford
  • Dean Henderson
  • James Trafford

Mabeki

  • Reece James
  • Tino Livramento
  • Nico O'Reilly
  • John Stones
  • Marc Guéhi
  • Ezri Konsa
  • Dan Burn
  • Jarell Quansah

Viungo

  • Declan Rice
  • Jude Bellingham
  • Jordan Henderson
  • Kobbie Mainoo
  • Elliot Anderson
  • James Garner
  • Eberechi Eze
  • Morgan Rogers

Washambuliaji

  • Harry Kane
  • Ivan Toney
  • Ollie Watkins
  • Bukayo Saka
  • Marcus Rashford
  • Anthony Gordon
  • Noni Madueke

Kundi la England Kombe la Dunia 2026

England imepangwa Kundi L pamoja na:

  • Croatia
  • Ghana
  • Panama

England itaanza kampeni yake ya Kombe la Dunia 2026 kwa kucheza dhidi ya Croatia tarehe 17 Juni 2026 katika mechi ya ufunguzi ya kundi hilo.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.