Matokeo ya michezo ya robo fainali mkondo wa kwanza wa UEFA Champions League yaliyochezwa usiku wa leo:
• Real Madrid 1–2 Bayern Munich
Mchezo huu uliokuwa na ushindani mkubwa umemalizika kwa Bayern Munich kuibuka na ushindi muhimu ugenini. Mabao ya Luis Díaz na Harry Kane ndio yaliyozamisha jahazi la Los blancos huku bao pekee la kufutia machozi likifungwa na Kylian Mbappé na kuhakikisha Bayern wanachukua ushindi huo muhimu kabla ya mechi ya marudiano itakayopigwa Allianz arena (Ujerumani).
• Sporting CP 0–1 Arsenal
Arsenal wamefanikiwa kupata ushindi mwembamba ugenini kupitia bao pekee la dakika za jioni la Kai Havertz, matokeo yanayowaweka katika nafasi nzuri kuelekea mchezo wa marudiano pale Emirates stadium (uingereza).
Kwa matokeo haya, Bayern Munich na Arsenal wanaondoka na faida muhimu, huku Real Madrid na Sporting CP wakilazimika kupambana zaidi katika michezo ya marudiano ili kugeuza matokeo.



